National Institute of Transport - NIT

LATEST NEWS

Thu, 16 Jan 2025 | 10:45 AM

NIT YASHEHEREKEA MAHAFALI YA 40, BODI YA WATAALAM WA SEKTA YA UCHUKUZI KUUNDWA

National Institute of Transport - NIT

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa masuala ya uchukuzi ipo katika hatua za kuandaa mapendekezo ya kutunga sheria ya Bodi ya wataalam wa Sekta ya Uchukuzi  kwa lengo la kuwatambua na kuwasajili wataalam wa Sekta hiyo.

Kauli hiyo imetolewa Desemba 20, 2024 na Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe.David Kihenzile katika mahafali ya 40 ya Chuo Cha Taifa cha Usafirishaji  (NIT), amesema bodi hiyo pia itakuwa na jukumu la kusimamia weledi na maadili ya watalaam wa Sekta ya Uchukuzi Tanzania Bara.

"Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo NIT, ipo katika hatua za kuandaa mapendekezo ya kutunga sheria ya Bodi ya Usajili wa Watalaam wa Sekta ya Uchukuzi , lengo la Bodi hii litakuwa kuwatambua, kuwasajili na kusimamia weledi na maadili ya wataalam wa Sekta ya Uchukuzi Tanzania Bara,"amesema Kihenzile.

Amesema uanzishwaji wa bodi hiyo una lengo la kuhakikisha  kazi zote za usafirishaji zinasimamiwa na watu wenye taaluma stahiki.

Akizungumzia kuhusu NIT, Kihenzile amesema  Serikali itaendelea kukiwezesha Chuo  ili kuhakikisha  kinatimiza majukumu yake ya kuandaa wataalam, kufanya tafiti na kutoa ushauri wa kitaalam katika sekta ya uchukuzi kwa maendeleo  endelevu ya Taifa letu.

"Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi, inafahamu vizuri mahitaji muhimu ya Chuo, ikiwa ni pamoja na ubora wa miundombinu ya kujifunzia, majengo, ofisi za wahadhiri na mabweni ya wanafunzi. Aidha, natambua kuwa Chuo kipo katika hatua za mwisho za kukamilisha ujenzi wa baadhi ya miundombinu hiyo kupitia mradi wa EASTRIP unaofadhiliwa na Benki ya Dunia(WB) ikiwemo mabweni ambayo nimejulishwa yamekamilika kwa asilimia 97 na majengo ya kituo cha Umahiri ya Usafiri wa Anga ambayo yamekamilika kwa asilimia 90.

"Napenda kuchukua nafasi hii kuuagiza Uongozi wa Chuo kuhakikisha miradi hii inakamilika kwa wakati ili ianze kutumika kwa kuwa mahitaji ni makubwa vilevile ninauagiza Uongozi kuendelea kutumia mapato ya ndani katika kuendeleza na kuboresha miundombinu ya Chuo,"amesisitiza Kihenzile.

Amesema amefarijika kusikia chuo kimeendelea kutanua wigo wa kutoa mafunzo katika sekta hii muhimu ya Uchukuzi, ikiwa ni pamoja na kujiimarisha katika Njia zote za Usafirishaji yaani Usafiri wa Anga, Maji, Reli, Barabara na Usafiri kwa njia ya mabomba. Mhe. Kihenzile pia amewataka wadau na wafaidika wa shughuli za chuo kwa pamoja na taasisi za umma na binafsi kuunga mkono jitihada za Chuo katika kutoa nafasi za mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi na kuendeleza bunifu zinazozalishwa chuoni ili ziweze kutumika kwa maendeleo ya nchi.

Awali Mkuu wa Chuo cha NIT, Mhandisi  Dkt. Prosper Mgaya amesema katika mahafali hayo  wahitimu 4176  wametunukiwa vyeti katika ngazi mbalimbali kati yao wanaume  ni 2,581 na wanawake 1,595.

"Kati ya wahitimu 4176 waliohitimu 29 wametunukiwa shahada ya Uzamili, 6 wametunukiwa statashahada ya uzamili,wahitimu 3,077 wametunukiwa shahada ya kwanza,wahitimu 36 wametunukiwa stashahada ya juu huku wahitimu 909 wametunukiwa stashahada ya kawaida, wahitimu 22  astashahada na wahitimu 22 wakitumikiwa astashahada ya awali,"amesema Dkt.Mgaya.

Akizungumzia  changamoto amesema Chuo kimekuwa na mikakati ya kukabiliana na changamoto mbalimbali  ikiwemo miundombinu na upungufu wa rasilimali watu sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi kwakuweka mikakati mbalimbali.

"Ili kukabiliana na upungufu wa miundombinu Chuo kimeendelea kujenga na kuboresha miundombinu ambapo kwa sasa kinaendelea na ujenzi wa mabweni mawili ambayo yatakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzo 1,500, ujenzi huu unatarajiwa kukamilika Januari 2025,"alisema Dk.Mgaya

Amesema sambamba na mabweni Chuo kinajenga ofisi, madarasa na karakana ambapo jumla ya majengo matatu yanajengwa na yanatarajiwa kukamilika Februari 2025 ambapo ujenzi huo unafadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia mradi wa EASTRIP.

Amesema chuo pia kinaanzisha kampasi mpya mkoani Lindi na Kilimanjaro ili kupunguza msongamano wa wanafunzi katika kampasi ya Dar es Salaam.

Kuhusu rasilimali watu amesema chuo kinaendelea kuomba vibali vya ajira mpya kwa watumishi kutoka Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kukabiliana na upungufu wa watumishi sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi. Ili kupunguza matumizi ya wahadhiri wa muda (Part-time lecturers).

astashahada na wahitimu 22 wakitumikiwa astashahada ya awali,"amesema Dkt.Mgaya.

Akizungumzia  changamoto amesema Chuo kimekuwa na mikakati ya kukabiliana na changamoto mbalimbali  ikiwemo miundombinu na upungufu wa rasilimali watu sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi kwakuweka mikakati mbalimbali.

"Ili kukabiliana na upungufu wa miundombinu Chuo kimeendelea kujenga na kuboresha miundombinu ambapo kwa sasa kinaendelea na ujenzi wa mabweni mawili ambayo yatakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzo 1,500, ujenzi huu unatarajiwa kukamilika Januari 2025,"alisema Dk.Mgaya

Amesema sambamba na mabweni Chuo kinajenga ofisi, madarasa na karakana ambapo jumla ya majengo matatu yanajengwa na yanatarajiwa kukamilika Februari 2025 ambapo ujenzi huo unafadhiliwa na Benki ya Dunia kupitia mradi wa EASTRIP.

Amesema chuo pia kinaanzisha kampasi mpya mkoani Lindi na Kilimanjaro ili kupunguza msongamano wa wanafunzi katika kampasi ya Dar es Salaam.

Kuhusu rasilimali watu amesema chuo kinaendelea kuomba vibali vya ajira mpya kwa watumishi kutoka Ofisi ya Raisi Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kukabiliana na upungufu wa watumishi sambamba na ongezeko la udahili wa wanafunzi. Ili kupunguza matumizi ya wahadhiri wa muda (Part-time lecturers).

 

Latest News

National Institute of Transport - NIT

ππˆπ“β€™π’ π…πˆπ‘π’π“ 𝐁𝐀𝐓𝐂𝐇 πŽπ… 𝐉𝐀𝐏𝐀𝐍𝐄𝐒𝐄 π’π‡πŽπ‘π“ π‚πŽπ”π‘π’π„ 𝐑𝐄𝐀𝐂𝐇𝐄𝐒 πŒπ€π‰πŽπ‘ πŒπˆπ‹π„π’π“πŽππ„

May 1, 2026, 9:50 a.m.

The National Institute of Transport (NIT), in collaboration with the Japan International Cooperation Agency (JICA) and the Organization for Technical Enhancement and Industrial Development (OTIDE), marked a significant milestone on 30th April 2026, as the first batch of students in its Japanese short course completed their training, with the ceremony held at the NIT Mabibo Campus.

Speaking during the graduation ceremony, NIT Rector Dr. Prosper Mgaya congratulated the students for their dedication and hard work. He encouraged them to continue strengthening their Japanese language skills and to apply them effectively in their future careers. He also noted the institute’s continued progress in aviation training, proudly highlighting that some graduates are already employed by airline companies as cabin crew. This course will also be a great advantage for aspiring cabin crew, as it equips them with the skills to interact confidently with diverse people, which is essential when applying and advancing in their future careers in aviation.

“We are immensely proud of this milestone you have achieved,” he said. “It reflects not only your academic success, but also your resilience, discipline, and unwavering commitment to personal growth.”

Representing OTIDE, Mr. Godwin Mbaga emphasized the importance of discipline and consistent practice in mastering a new language. He noted that strong language proficiency can create wide-ranging career opportunities for students.

“On her part, Ms. Minako Yamamoto, Senior Representative of JICA, commended the graduates for their commitment and resilience. She underscored the growing partnership between Japan and Tanzania and encouraged them to continue improving their Japanese language skills in order to maximize future opportunities.”

“Completing this course was not easy, especially with your busy schedules,” she said. “I am impressed that you were able to finish. It is not only what you achieve that matters, but how you achieve please stay committed.”

National Institute of Transport - NIT

πŒπ€π…π”ππ™πŽ π˜π€ π•πˆπ πŠπ–π€ πŒπ€πƒπ„π‘π„π•π€ 𝐖𝐀 π‰π„π’π‡πˆ 𝐋𝐀 ππŽπ‹πˆπ’πˆ π˜π€π…π”ππ†π–π€ π‘π€π’πŒπˆ

May 1, 2026, 9:48 a.m.

Naibu Mkuu wa Chuo Mipango, Fedha na Utawala - NIT, Dkt. Dkt.Zainabu Mshana amefunga rasmi mafunzo ya VIP yaliyoandaliwa kwaajili madereva wanaoendesha viongozi wa jeshi la polisi tarehe 30 Aprili 2026.

Akizungumza na madereva waliohudhuria mafunzo hayo kutoka jeshi la polisi wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo iliyofanyika katika ukumbi wa Auditorium uliyopo katika kampasi ya Chuo Mabibo Jijini Dar es salaam Dkt. Mshana amelishukuru Jeshi la Polisi kwa kuchagua NIT kama sehemu sahihi kwa madereva hao kupatiwa mafunzo ya VIP daraja la pili.

"Kwa niaba ya Uongozi wa Chuo natoa shukrani za dhati kwa Uongozi wa Jeshi la Polisi nchini kwa kuleta madereva hawa NIT kupata mafunzo haya ambayo ni muhimu kwaajili kuhakikisha viongozi wetu wanakuwa salama"

Aidha, Dkt.Mshana ametoa wito kwa madereva walioshiriki mafunzo hayo kuzingatia yote waliyofundishwa kwa kuzingatia maadili ya kazi na sheria za usalama barabarani.

"Ni matumaini yangu baada ya kuhitimu mafunzo haya mtakuwa mabalozi wazuri kwa kutekeleza majukumu yenu kwa weledi na kuzingatia sheria za usalama barabarani.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkuu wa Chuo cha Maafisa wa Jeshi la Polisi SCP.Deus Sokoni ameushukuru Uongozi wa Chuo pamoja na wakufunzi wa Chuo kwa kuandaa mafunzo ya VIP kwa madereva wa Jeshi la Polisi.

Mafunzo ya VIP daraja la pili kwa madereva wanaoendesha viongozi wa Jeshi la Polisi yalianza tarehe 1 hadi 30 Aprili 2026 ambapo jumla ya madereva hamsini (50) kutoka Jeshi la Polisi wamehudhuria na kutunukiwa vyeti.

National Institute of Transport - NIT

π–π€π…π€ππ˜π€πŠπ€π™πˆ ππŽπ‘π€ 𝐍𝐀 π‡πŽπƒπ€π‘πˆ ππˆπ“ πŒπ–π€πŠπ€ 𝐖𝐀 𝐅𝐄𝐃𝐇𝐀 πŸπŸŽπŸπŸ“/πŸπŸŽπŸπŸ” π–π€πŠπ€ππˆπƒπ‡πˆπ–π€ π™π€π–π€πƒπˆ

May 1, 2026, 9:47 a.m.

Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Mha.Dkt. Prosper Mgaya amekabidhi zawadi mbalimbali kwa wafanyakazi bora na hodari wa Chuo kwa mwaka wa fedha 2025/2026. Watumishi hao wamekabidhiwa zawadi zao ikiwemo fedha taslimu na vyeti tarehe 30 Aprili 2026.

Akizungumza na watumishi wa Chuo wakati wa hafla fupi ya kukabidhi zawadi kwa wafanyakazi bora na hodari iliyofanyika katika ukumbi wa MPH uliyopo katika kampasi ya Chuo Mabibo Jijini Dar es salaam Dkt. Mgaya amewapongeza wafanyakazi kazi hao kwa kuibuka washindi katika zoezi la kuchagua wafanyakazi bora na hodari wa Chuo lililofanyika hivi karibuni baada ya kuidhinishwa kwa Mwongozo wa Jinsi ya Kumpata Mfanyakazi Bora na Mfanyakazi Hodari wa Chuo.

"Kwa niaba ya Uongozi wa Chuo nawapongeza watumishi wote waliochaguliwa kuwa wafanyakazi bora na hodari katika mwaka huu wa fedha,huu ni mwanzo mzuri natumaini mtakiwakilisha vizuri Chuo katika zoezi la utoaji wa tuzo wakati wa Maadhimisho ya Sikukuu ya Wafanyakazi Duniani kitaifa"

Aidha, Dkt.Mgaya amewahakikishia watumishi wa Chuo kuwa zoezi la kutoa motisha mbalimbali kwa wafanyakazi bora na hodari wa Chuo kuwa endelevu na kuboreshwa zaidi.

"Huu ni mwanzo tuu, tutaendelea na utaratibu huu mwakani na kufanya maboresho mbalimbali"

Zoezi la kuchagua wafanyakazi bora na hodari wa Chuo limehitimishwa leo kwa washindi kutangazwa na kukabidhiwa zawadi zao ambapo Mha.Castor Njako ameibuka mfanyakazi hodari wa Chuo, Bi.Rehema Mzee (mfanyakazi bora kada ya wanataaluma),Bw.Meshack Kimaro(mfanyakazi bora kada ya waendeshaji),na wafanyakazi bora katika kundi la ushindani akiwemo Bw.Honest Mrosso, aBw.Robert Kilamato,Bw.Michael Soka,Bw.Juma Msemwa, na CPA.Innocent Mshanga.