Wed, 18 Jun 2025 | 01:25 PM
Chuo cha Taifa cha Usafirishaji kimewaapisha viongozi wapya wa Serikali ya Wanafunzi Students` Organization National Institute of Transport (SONIT) kwenye hafla fupi ya uapisho ilifanyika Jumanne tarehe 17 mwezi huu katika viwanja vya NIT Mabibo Campus.
Akizungumza katika hafla hiyo Mkuu wa Chuo Dkt. Prosper Mgaya ameipongeza Serikali iliyomaliza muda wake kwa kuwa kiunganishi kizuri baina ya Uongozi wa Chuo na Wanafunzi na hivyo kupelekea kurahisisha utendaji kazi na kusaidia Wanafunzi kusoma kwa amani na utulivu.
Aidha Dkt. Mgaya ameipongeza kurugenzi ya huduma za wanafunzi ya NIT kwa kuwasimamia vizuri wanafunzi hao katika mambo mbalimbali wanapokua hapa Chuoni. ``Ninyi ndio mko na hawa wanafunzi mara nyingi na kwa kuwa wameonesha nidhamu ya hali ya juu katika maisha yao hapa Chuoni sina budi kuwapongeza sana kwa kuwasimamia vema``. Amesema
Kwa upande wake Rais wa Serikali ya Wanafunzi iliyomai za muda wake Bw. Stavius Alkad amesema katika kipindi cha uongozi wake alipata ushirikiano mkubwa kutoka kwa Uongozi wa Chuo na kwamba amejifunza mambo mengi ya kiuongozi na kuwasihi viongozi wanaongia madarakani kushirikiana vizuri na Uongozi wa Chuo ili wachote busara alizopata yeye
Katika hatua nyingine Dkt. Mgaya amezindua viti vya zege vya kusomea Wanafunzi maarufu kama ``Vimbweta`` vilivyojengwa na Serikali ya SONIT iliyomaliza muda wake, viti hivyo vya kisasa vitawawezesh wanafunzi kusoma hata nyakati za usiku kwani vimefunikwa kwa paa na kuwekwa umeme. Hii ni hatua kubwa sana ambayo Serikali iliyopita imeionesh kama mfano, ni matumaini yangu kuwa Serikali tulioiapisha hivi leo itafanya mambo mengine mkubwa zaidi ukizingatia Rais wa sasa alikua ni Waziri Mkuu katika Serikali iliyopita.
Katika hafla hiyo iliyojaa shamrashamra na maatumaini makubwa kwa wanafunzi juu ya Uongozi mpya ulioapishwa, Mkufunzi wa michezo wa Chuo Bw. Augustino Saquare alikabidhi makombe mawili ambayo timu za wanafunzi zilishinda katika Mashindano ya SHMIVUTA na yale ya SEPESHA RUSHWA yaliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana na timu hizo kuibuka kidedea katika nafasi mbalimbali.