National Institute of Transport - NIT
Bonyeza Kuthibitisha

ALL NEWS

All News

National Institute of Transport - NIT

NAIBU KATIBU MKUU - WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI ZANZIBAR AIPONGEZA NIT

July 18, 2025, 2:20 p.m.

Tarehe 16 Julai 2025, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elim una mafunzo ya Amali Zanzibar Bw. Khalid Masoud Wazir alitembelea banda la Chuo cha Taifa cha usafirishaji (NIT) katika Maonesho ya sita ya Wiki ya Elimu ya Juu yanayoendelea katiika viwanja vya Mnazi Mmoja, Unguja -Zanzibar.

Katika ziara hiyo Bw. Wazir ameipongeza NIT kwa kazi nzuri inayofanya katika utoaji mafunzo, ushauri wa kitaalamu na utafiti. Aidha, amehimiza kuendelea kutoa ushauri wa kitaalamu na kuelimisha wanafunzi kuhusu namna ya kuchagua kozi sahihi kwa maendeleo yao ya kitaaluma, kulingana na ufaulu wao.

Kwa niaba ya Mkuu wa Chuo cha NIT, Dkt. Prosper Mgaya, Kaimu Mkurugenzi Huduma Saidizi Taaluma Bi.Adela Muhale alimshukuru Naibu Katibu kwa kutembelea banda na akaahidi Chuo kuendelea kushirikiana na Serikali ili kuhakikisha malengo ya elimu yanafakiwa kwa ufanisi.

Maonesho ya 6 ya Wiki ya Elimu ya Juu yanaendelea viwanja vya Mnazi Mmoja- Zanzibarkuanzia tarehe 14-20 Julai 2025

National Institute of Transport - NIT

WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI ZANZIBAR ATEMBELEA BANDA LA NIT

July 18, 2025, 2:18 p.m.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Mhe. Lela Mohamed Mussa, ametembelea banda la NIT katika Maonesho ya 6 ya Wiki ya Elimu ya Juu katika Kilele cha maonesho hayo leo tarehe 17.7.2025 kama Mgeni Rasmi Mnazi Mmoja, Zanzibar.

Akizungumza katika ziara hiyo, Mhe. Lela amesisitiza umuhimu wa kuunganisha elimu ya kitaaluma na mafunzo ya vitendo, akisema Serikali itaendelea kuwekeza katika taasisi kama NIT ambayo inalenga kutoa ujuzi unaokidhi mahitaji ya soko la kazi.

Amesisitiza kuwa elimu si tu maarifa ya kitabiri bali inapaswa kuwa lango la kutoa ajira na kukuza ubunifu nchini.
Kwa niaba ya Mkuu wa Chuo cha NIT, Dkt. Prosper Mgaya, Kaimu Mkurugenzi Huduma Saidizi Taaluma Bi.Adela Muhale alimueleza Mhe. Waziri kuhusu programu mbalimbali za Mafunzo zinazotolewa Chuoni. Waziri alipongeza Chuo kwa mafanikio yaliyopo na kuhimiza Chuo kuendelea na ubunifu katika elimu ya vitendo.

Maonesho ya Wiki ya Elimu ya Juu ya mwaka huu yanakusudia kukuza ushirikiano kati ya vyuo vikuu, taasisi za ufundi na sekta binafsi ili kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata ujuzi unaohitajika kutimiza ajira.

Maonesho ya 6 ya Wiki ya Elimu ya Juu yanaendelea viwanja vya Mnazi Mmoja- Zanzibarkuanzia tarehe 14-20 Julai 2025

National Institute of Transport - NIT

WANAFUNZI WA UHUDUMU NDANO YA NDEGE WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO JNIA

July 18, 2025, 2:17 p.m.

Wanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji wanaosoma kozi ya muda mfupi ya Uhudumu ndani ya Ndege wametembelea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwl.Nyerere tarehe 17 Julai, 2025 ikiwa ni sehemu ya mafunzo yao kwa vitendo

National Institute of Transport - NIT

DKT. MGAYA AFUNGUA SEMINA ELEKEZI KWA VIONGOZI WA SERIKALI TA WANAFUNZI

July 18, 2025, 2:16 p.m.

Mkuu wa Chuo Dkt. Prosper Mgaya amefungua semina elekezi ya siku mbili (2) ya Viongozi wateule wa Serikali ya Wanafunzi,Students’ Organisation of National Institute of Transport (SONIT) leo tarehe 17 Julai, 2025.

Akizungumza wakati wa ufunguzi Dkt. Mgaya amewaasa viongozi hao kutilia maanani mafunzo hayo kwani ni akiba yao ya siku zijazo ``Viongozi wengi wakubwa walianzia kwenye ngazi ya Chuo au Shuleni hivyo mafunzo ya namna hii siyo ya kuyapuuzia hata kidogo kwani yanaweza kuwasaidia siku zijazo endapo hayatakusaidia kwa sasa``. Amesema

Semina hiyo iliyoandaliwa na Kurugenzi ya Huduma za Wanafunzi ya Chuo imeandaa mada mbalimbali zikiwemo za kupambana na Rushwa ,kufahamu maadili ya kiuongozi na mada zinazohusiana na masuala ya Afya ya akili.

Akizungumzia sababu ya kuandaa mada hizo Mkurugenzi wa Huduma za wanafunzi Ndg. Abel Luzibila amesema kutokana na mabadiliko ya mara kwa mara katika Ulimwengu wa sasa ni vizuri Viongozi kujua juu ya mambo mbalimbali kuhusiana na afya ya akili kwani ni changamoto inalojitokeza sana kwa vijana walio vyuoni .
Ndg. Luzibila amesema tumewaalika watoa mada kutoka Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa, Chuo kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi na Wakufunzi wa hapa kwetu ili kuhakikisha mada zinazotolewa zinatolewa kwa weledi wa hali ya juu.

National Institute of Transport - NIT

3rd International Conference on Transport, Logistics, and Management

July 2, 2025, 9:20 a.m.

The National Institute of Transport (NIT) is organizing the 3rd International Conference on Transport, Logistics, and Management. Its main objective is to create a platform for Transport, Logistics, and  Management professionals to share research findings/results and experiences; and discuss solutions for Transport and Logistics challenges. The Conference's main theme is "Harnessing Innovative and Sustainable Transport Systems for Enhanced Mobility and Safety".

Main Theme: Harnessing Innovative and Sustainable Transport Systems for Enhanced Mobility and Safety.

Click the link below for Registration:-

Event Registration Form

National Institute of Transport - NIT

๐—ž๐—”๐—ง๐—œ๐—•๐—จ ๐— ๐—ž๐—จ๐—จ ๐—จ๐—–๐—›๐—จ๐—ž๐—จ๐—ญ๐—œ ๐—”๐—™๐—จ๐—ก๐—š๐—จ๐—” ๐—ž๐—œ๐—ž๐—”๐—ข ๐—–๐—›๐—” ๐—•๐—”๐—ฅ๐—”๐—ญ๐—” ๐—Ÿ๐—” ๐—ช๐—”๐—™๐—”๐—ก๐—ฌ๐—”๐—ž๐—”๐—ญ๐—œ ๐—ก๐—œ๐—ง ๐— ๐—ž๐—ข๐—”๐—ก๐—œ ๐——๐—ข๐——๐—ข๐— ๐—”

June 27, 2025, 5:41 p.m.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimefanya kikao cha kawaida cha Baraza la Wafanyakazi tarehe 27 Juni, 2025 katika Ukumbi wa Midland Inn View Hotel, Dodoma. Kikao hicho kilitanguliwa na kikao cha Kamati ya Utendaji kilichofanyika Juni 26, 2025.

Kikao hicho kilifunguliwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara, ambaye alikipongeza chuo kwa kuandaa vikao vinavyodumisha ushirikiano wa watumishi na uongozi. Alisisitiza kuwa NIT iendelee kuzalisha wataalamu kutokana na ukuaji wa sekta ya usafirishaji unaoletwa na miradi kama SGR na ongezeko la ndege za ATCL. Aidha, alihimiza ushirikiano na vyuo vya nje kwa ajili ya maendeleo ya kiteknolojia.

Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo, Prof. Obadia Mbamba, alishukuru Wizara kwa ushirikiano wake unaosaidia ustawi wa chuo. Viongozi wa vyama vya wafanyakazi wa THTU na RAAWU Taifa waliupongeza uongozi wa NIT kwa maandalizi bora ya kikao na kutoa motisha kwa watumishi (incentive) inayoongeza morali ya kazi.

Mkuu wa Chuo, Dkt. Prosper Mgaya, alimshukuru Prof. Kahyarara kwa kuwa mgeni rasmi na kuahidi kuendeleza vikao hivyo kwa kuzingatia sheria na kanuni husika.

National Institute of Transport - NIT

๐๐ˆ๐“ ๐˜๐€๐“๐Ž๐€ ๐Œ๐€๐…๐”๐๐™๐Ž ๐˜๐€ ๐”๐’๐€๐‹๐€๐Œ๐€ ๐๐€๐‘๐€๐๐€๐‘๐€๐๐ˆ ๐Š๐–๐€ ๐Œ๐€๐ƒ๐„๐‘๐„๐•๐€ ๐–๐€ ๐•๐˜๐Ž๐Œ๐๐Ž ๐•๐˜๐€ ๐Œ๐Ž๐“๐Ž ๐Œ๐Š๐Ž๐€ ๐–๐€ ๐๐–๐€๐๐ˆ.

June 26, 2025, 11:29 a.m.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), kupitia Kituo chake cha Kikanda cha Umahiri katika Usalama Barabarani (RCoERS), kimeanza kutoa mafunzo maalum ya usalama barabarani kwa madereva wa magari makubwa ya mizigo, daladala na bodaboda katika Mkoa wa Pwani.

Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo yaliyofanyika tarehe 24 Juni, 2025 katika Stendi Kuu ya Mabasi ya Kibaha, Mkuu wa Kituo cha Umahiri cha Kikanda cha Usalama Barabarani – NIT, Ndg. Godlisten Msumanje, alisema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo madereva hao kutekeleza majukumu yao kwa weledi, huku wakizingatia sheria na kanuni za usalama barabarani ili kulinda usalama wao pamoja na wa abiria wanaowahudumia.

“NIT imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya usafirishaji nchini kutoa elimu endelevu ya usalama barabarani kwa makundi mbalimbali katika jamii ili kuongeza uelewa wa usalama barabarani kwa watumiaji wote wa barabara,” alisisitiza Ndg. Msumanje.

Mafunzo haya yalianza rasmi tarehe 23 Juni, 2025 na yanatarajiwa kukamilika tarehe 27 Juni, 2025.

National Institute of Transport - NIT

๐Ÿฎ๐Ÿฌ ๐—ง๐—”๐—ก๐—ญ๐—”๐—ก๐—œ๐—”๐—ก ๐—ฆ๐—ง๐—จ๐——๐—˜๐—ก๐—ง๐—ฆ ๐—š๐—ฅ๐—”๐——๐—จ๐—”๐—ง๐—˜ ๐—™๐—ฅ๐—ข๐—  ๐—ก๐—œ๐—งโ€“๐—ž๐—œ๐—›๐—•๐—ง ๐—๐—ข๐—œ๐—ก๐—ง ๐—˜๐—ก๐—š๐—œ๐—ก๐—˜๐—˜๐—ฅ๐—œ๐—ก๐—š

June 26, 2025, 11:25 a.m.

oday, June 24, 2025, twenty (20) Tanzanian students graduated from a six-month joint engineering program between the National Institute of Transport (NIT) and the Kenya Institute of Highways and Building Technology (KIHBT) at the NIT Mabibo Campus.

Speaking during the graduation ceremony, Dr. Prosper Mgaya, Rector of NIT, announced that NIT and KIHBT formalized their partnership by signing a Memorandum of Understanding in October 2023 in Nairobi, Kenya. This collaboration operates under the umbrella of the World Bank's East Africa Skills for Transformation and Regional Integration Project (EASTRIP). Dr. Mgaya stated that following the signing, discussions focused on implementing a student exchange and mobility program to fulfill EASTRIP's requirement for regional enrollment in long-course programs.

On his side Dr. Chacha Ryoba, Center Leader of the NIT Center of Excellence in Transport Operations under EASTRIP, elaborated on the program structure. He stated that each institution enrolled twenty students in two distinct programs: Power Train and Suspension Systems and Construction Material and Testing.

NIT students completed a one-month in-person phase of the program in Kenya, followed by five months of online instruction delivered by KIHBT lecturers. Conversely, KIHBT students completed a one-month in-person phase in Tanzania, followed by five months of online instruction delivered by NIT lecturers. While the Kenyan students graduated on June 19, 2025, the Tanzanian students received their certifications today, June 24, 2025. The graduates expressed optimism and enthusiasm for their future endeavors in the engineering field.

KALENDA YA KOZI ZA MADEREVA JUNE โ€“ DESEMBER 2025

June 25, 2025, 10:23 a.m.

National Institute of Transport - NIT

KATIBU MKUU UTUMISHI ATEMBELEA BANDA LA NIT DODOMA

June 18, 2025, 4:21 p.m.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Mhe. Juma S. Mkomi ametembelea banda la Chuo tarehe 18.6.2025 lililopo katika viwanja vya Maonesho vya Chinangali jijini Dodoma.

Akiwa katika banda la Chuo Mhe. Mkomi amekipongeza Chuo kwa kuanzisha mafunzo ya kimkakati nchini ikiwemo mafunzo  ya urubani.

Wiki ya Utumishi wa Umma huadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kutambua mchango wa watumishi wa umma katika maendeleo ya jamii.

Maadhimisho hayo yataendelea hadi tarehe 23 Juni, 2025 yakihusisha utoaji wa elimu na huduma mbalimbali.

50 YEARS NIT ANNIVERSARY 1975-2025

Excellence in Transport for a Sustainable Economy.