National Institute of Transport - NIT
Bonyeza Kuthibitisha

ALL NEWS

All News

National Institute of Transport - NIT

VIONGOZI SERIKALI YA WANAFUNZI WAAPISHWA

June 18, 2025, 1:25 p.m.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji kimewaapisha viongozi wapya wa Serikali ya Wanafunzi Students` Organization National Institute of Transport (SONIT) kwenye hafla fupi ya uapisho ilifanyika Jumanne tarehe 17 mwezi huu katika viwanja vya NIT Mabibo Campus.

Akizungumza katika hafla hiyo Mkuu wa Chuo Dkt. Prosper Mgaya ameipongeza Serikali iliyomaliza muda wake kwa kuwa kiunganishi kizuri baina ya Uongozi wa Chuo na Wanafunzi na hivyo kupelekea kurahisisha utendaji kazi na kusaidia Wanafunzi kusoma kwa amani na utulivu.

Aidha Dkt. Mgaya ameipongeza kurugenzi ya huduma za wanafunzi  ya NIT kwa kuwasimamia vizuri wanafunzi hao katika mambo mbalimbali wanapokua hapa Chuoni. ``Ninyi ndio mko na hawa wanafunzi mara nyingi na kwa kuwa wameonesha nidhamu ya hali ya juu katika maisha yao hapa Chuoni sina budi kuwapongeza sana kwa kuwasimamia vema``. Amesema

Kwa upande wake Rais wa Serikali ya Wanafunzi iliyomai za muda wake Bw. Stavius Alkad amesema katika kipindi cha uongozi wake alipata ushirikiano mkubwa kutoka kwa Uongozi wa Chuo na kwamba amejifunza mambo mengi ya kiuongozi na kuwasihi viongozi wanaongia madarakani kushirikiana vizuri na Uongozi wa Chuo ili wachote busara alizopata yeye

Katika hatua nyingine Dkt. Mgaya amezindua viti vya zege vya kusomea Wanafunzi maarufu kama ``Vimbweta`` vilivyojengwa na Serikali ya SONIT iliyomaliza muda wake, viti hivyo vya kisasa vitawawezesh wanafunzi kusoma hata nyakati za usiku kwani vimefunikwa kwa paa na kuwekwa umeme. Hii ni hatua kubwa sana ambayo Serikali iliyopita imeionesh kama mfano, ni matumaini yangu kuwa Serikali tulioiapisha hivi leo itafanya mambo mengine mkubwa zaidi ukizingatia Rais wa sasa alikua ni Waziri Mkuu katika Serikali iliyopita.

Katika hafla hiyo iliyojaa shamrashamra na maatumaini makubwa kwa wanafunzi juu ya Uongozi mpya ulioapishwa, Mkufunzi wa michezo wa Chuo Bw. Augustino Saquare alikabidhi makombe mawili ambayo timu za wanafunzi zilishinda katika Mashindano ya SHMIVUTA na yale ya SEPESHA RUSHWA yaliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana na timu hizo kuibuka kidedea katika nafasi mbalimbali.

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI NIT JUNE 2025

June 9, 2025, 7:15 p.m.

SHORTLISTED PILOT TRAINING APPLICANTS

May 28, 2025, 1:16 p.m.

National Institute of Transport - NIT

INVITATION FOR APPLICATIONS OF PRIVATE PILOT LICENSE (PPL) COURSE

May 14, 2025, 9:30 a.m.

The National Institute of Transport is proud to announce the launching of our first ever Private Pilot License (PPL) Course, designed to provide comprehensive aviation training for aspiring pilots. The course is approved by the Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA) through Approval Number TCAA/ATO/010.

 

Click the link for Applying: https://aviation.nit.ac.tz/index.php/login/

National Institute of Transport - NIT

ZIARA YA NAIBU KATIBU MKUU - UCHUKUZI

May 13, 2025, 11:44 a.m.

Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Ludovick Nduhiye  ameutaka uongozi wa chuo cha Taifa cha Usafiraji (NIT) kuhakikisha wanatunza na  kuendeleza vifaa kwa ajili ya mafunzo ya Urubani, Wahudumu wa ndani ya Ndege na Wahandisi Matengenezo ya ndege.

Nduhiye amesema  hayo tarehe 9.5.2025 baada ya kutembelea na kukagua vifaa mbalimbali vilivyonunuliwa na Serikali katika kufundishia mafunzo ya Marubani na Wahudumu wa ndani ya Ndege.

“Serikali imewekeza fedha nyingi katika kununua vifaa hivyo vya kufundishia marubani hivyo uongozi wa Chuo unatakiwa kuhakikisha vifaa hivi vinatunzwa ili vidumu kwa muda mrefu” Alisema Nduhiye.

Pamoja na kukagua  na kutembelea vifaa hivyo pia alikagua ujenzi wa hosteli za wanafunzi wa kike na wakiume  majengo ya utawala ambayo ujenzi wake umefikia asilimia 98 na unatarajiwa kukamilika katika mwaka huu.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Dkt. Prosper Mgaya amesema kuwa vifaa vyote vya  kufundisha urubani katika chuo  vimekamilika na mafunzo hayo yanatarajia kuanza Mwezi sita  mwaka huu. Aidha ameushukuru Uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali yote kwakuwa wamewezesha ununuzi wa vifaa hivyo.

“ Vifaa vya kufundishia Urubani vimekamilika na tumeshapata idhini kutoka mamlaka ya Usimamizi wa Anga (TCAA) kuanza kufundisha hivyo tunatarajia kuanza kutoa mafunzo haya mwezi wa sita na tuanza na wanafunzi kumi na mbili” Alisema Mgaya

 Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo hicho Prof. Ulingeta Mbamba amesema Baraza la chuo litaendelea kusimamia  Ubora  wa Elimu unaotolewa na chuo hicho kwa masomo yaote ili chuo hicho kiendelee kutoa wataalam wanaoweza kushindana katika soko la ajira za ndani na nje ya nchi.

Mkufunzi wa Mafunzo ya wahudumu wa ndani ya Ndege amesema kuwa vifaa vyote vya wahudumu wa ndege vipo tayari kwa ajili ya kufundishia hivyo anawakaribisha  vijana   kwenda katika chuo hicho kupata mafunzo hayo katika Sekta ya Anga.

National Institute of Transport - NIT

NIT GRADUATE EXIT PROGRAMME

May 13, 2025, 11:41 a.m.

National Institute of Transport (NIT) conducted a graduate exit programme at the NIT Mabibo Campus. This programme, among other things, is designed to better prepare graduates for the employment market.
Speaking at the inauguration of the programme, the Acting Deputy Rector for Academic Research and Consultancy, Dr. Eva Luhwavi, stated that today is indeed another significant occasion in your academic careers, during which the Institute is equipping you to more effectively navigate the job market. This event elicits a range of emotions in graduating students: delight in expectation of embarking upon a new chapter in their lives and, for others, pleasure and satisfaction with their accomplishments.
"And we, as the Institute, also take pride in your achievements. Concurrently, we bear the responsibility of working tirelessly and continuing to enhance the quality of our training and to develop contemporary teaching and research methods," Dr. Luhwavi added. "I would like to take this opportunity to congratulate all the students who will graduate in this academic year of 2024/2025. You have undertaken a considerable journey here at the NIT, with some of you having spent four years and others three. I sincerely request that the time you have invested at the Institute has not been in vain, so that you may proceed to contribute effectively wherever you may go.
"We are all aware that human resources constitute one of the most crucial foundations in establishing a modern and efficient society. Therefore, I would advise all of you who are graduating to utilise the knowledge you have acquired, each within your respective discipline, to foster the development of our nation."
Dr. Luhwavi Concluded, I would implore employers and parents to give these graduates opportunities so that they may demonstrate their proficiency. There is a tendency to favour the recruitment of young individuals with prior experience. I assure you that our young people have undergone practical training, and thus, despite their potential lack of experience in a professional environment, they possess the skills necessary to apply in the roles they will secure. Indeed, I believe in their capabilities"

National Institute of Transport - NIT

NIT YAKABIDHIWA NDEGE YA MAFUNZO NA NCCA

April 24, 2025, 4:20 p.m.

MAMLAKA ya Uhifadhi Ngorongoro (NCAA) imekabidhi ndege ya mafunzo kwa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) ili kuunga mkono jitihada za Serikali kuongeza wataalamu wa urushaji wa ndege. Makabidhiano hayo yamefanyika jijini Dodoma tarehe 24.4.2025.

Akizungumza baada ya kukabidhi ndege hiyo Kamishna Msaidizi mwandamizi wa Ngorongoro Salma Chisonga alisema ndege hiyo itasaidia kuongeza wataalamu wa kurusha ndege ambao watalisaidia Taifa.

National Institute of Transport - NIT

NIT YATOA MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI KWA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI WILAYA YA KASULU MKOANI KIGOMA

March 26, 2025, 9:57 a.m.

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kupitia Kituo chake cha Kikanda cha Umahiri katika Usalama Barabarani kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Wilaya ya Kasulu Kitengo cha Usalama Barabarani - Dawati la Elimu  kimeanza kutoa mafunzo ya siku tano (5) ya usalama barabarani yanayolenga wanafunzi wa shule za msingi, madereva wa bodaboda, bajaji na magari madogo ya abiria  wa Wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma.

Akizungumza na waandishi habari baada ya mafunzo hayo yaliyoanza rasmi tarehe 17.3.2025 katika shule za msingi za Murubona, Kalema, Kigamano, Umoja na Kimobwa, Mkuu wa Kituo cha  
Kikanda cha  Umahiri katika Usalama Barabarani - NIT, Ndg. Godlisten Msumanje amesema lengo la mafunzo hayo ni kuelimisha wanafunzi wa shule za msingi, madereva wa bodaboda, bajaji na magari madogo ya abiria  kuhusu matumizi salama na sahihi ya barabara ili kusaidia kupunguza ajali na kuboresha usalama wa watumiaji wa barabara.

Kwa upande wa wanafunzi waliopatiwa mafunzo hayo   wamekishukuru Chuo kwa kutoa mafunzo hayo na kuahidi kuwa mabalozi wazuri wa usalama barabarani kwa kuwaelimisha wenzao.

PRESS RELEASE

March 11, 2025, 11:38 a.m.

KUWASILISHA MAOMBI YA KUISHI KATIKA HOSTEL ZA CHUO

Feb. 20, 2025, 12:22 p.m.

50 YEARS NIT ANNIVERSARY 1975-2025

Excellence in Transport for a Sustainable Economy.