Aug. 30, 2024, 9:01 a.m.
Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kupitia kituo chake cha Umahiri cha Kikanda Katika Usalama Barabarani kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Kitengo cha Elimu ya Usalama Barabarani kimetoa Mafunzo ya Usalama Barabarani Mkoani Dodoma.
Mafunzo hayo yamefanyika tarehe 28.8.2024 na 29.8.2024 wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani kwa wanafunzi wa shule za msingi kumi na moja(11) ikiwemo shule ya msingi Mazengo ,Kikuyu,Amani,Mlezi, Mlimani, Makole, Kizota, Chadulu, Mlimwa, na Kisasa.
Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea wanafunzi hao uwelewa wa matumizi sahihi ya barabara.
Aug. 30, 2024, 8:59 a.m.
Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kupitia kituo chake cha Umahiri cha Kikanda katika Usalama Barabarani (Regional Centre of Excellence for Road Safety) imetoa Mafunzo ya Udereva wa Magari ya Mizigo (HGV) kwa madereva kumi na nne (14).
Mafunzo hayo yameanza tarehe 19.08.2024 na yanatarajia kumalizika tarehe 31.08.2024 katika Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani Mkoani Dodoma
Lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo na umahiri madereva hao katika kuendesha magari ya mizigo kwa kuzingatia sheria na kanuni za usalama barabarani.
Aug. 30, 2024, 8:57 a.m.
Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimeibuka mshindi wa kwanza (1) kati ya Taasisi kumi na moja(11) za Elimu ya Juu ambazo zimeshiriki kwenye maonesho ya kongamano la tisa 9 la wahandisi wanawake Tanzania (Tawece) na kukabidhiwa tuzo ya mshindi wa kwanza.
Kongamano hilo limefanyika jijini Dar es salaam katika Ukumbi wa Julius Nyerere International Convention Center (JNICC) kuanzia tarehe 21 hadi 22 Agosti,2024.
Mkuu wa Idara ya ππ‘πππ©π§π€π£πππ¨ ππ£π πππ‘πππ€π’π’πͺπ£ππππ©ππ€π£ ππ£πππ£πππ§ππ£π Bi. Grace Kibweja amepokea tuzo hiyo ya mshindi wa kwanza kwa niaba ya Mkuu wa Chuo.
July 17, 2024, 9:31 a.m.
July 5, 2024, 2:03 p.m.
The National Institute of Transport (NIT) is offering intensive review classes to help you prepare for the Certified Public Accountant (CPA) and Certified Procurement and Supply Professional (CPSP) examinations in November 2024.
For registration, please click the link https://shorturl.at/sBYpq
For payment purposes contact the coordinators:
Head CPD Mobile: +255713323370 or Assistant Head CPD Mobile +255719589955
Email: head.cpd@nit.ac.tz
June 22, 2024, 9:03 a.m.
June 8, 2024, 10:41 p.m.
Chuo cha Taifa cha Usafirishaji chaendelea kutoa mafunzo kwa Wahudumu wa Mabasi ya Masafa Marefu na Mijini - Dar es salaam. Mafunzo hayo ya siku sita (6) yalianza siku ya Jumatatu tarehe 03.06.2024 na kuhitimishwa siku ya Jumamosi tarehe 08.06.2024 ambapo jumla ya washiriki 43 wemehudhuria mafunzo hayo na kutunukiwa vyeti.
Akizungumza na washiriki wakati wa Hafla ya Kufunga Mafunzo hayo iliyofanyika leo katika ukumbi wa Kituo cha Ukaguzi wa Magari uliyopo katika kampasi ya Chuo Mabibo jijini Dar es salaam, Kaimu Mkuu wa Chuo Taaluma, Utafiti na Ushauri Elekezi, Dkt. John Mahona
amewaasa washiriki wa mafunzo hayo kuzingatia yale yote
waliyojifunza ili kuleta tija na mabadiliko chanya katika vituo vyao vya kazi. Amesema
"Mkayazingatie yote mliyofundishwa ili kuleta tija katika vituo vyenu vya kazi"
June 8, 2024, 10:36 p.m.
NIT students participated in a one-day workshop organized by the Carter Center in collaboration with China-Africa Vocational Education Cooperation Alliance (CAVECA).
The workshop was held at NIT main campus Mabibo Dar es Salaam on Saturday 8th June 2024 focusing on empowering students with knowledge on the importance of climate - resilient infrastructure such as flood plains, embankments and other systems to reduce vulnerability to climate -related hazards such as floods and landslides.
June 7, 2024, 11:44 a.m.
June 5, 2024, 12:08 p.m.
Mkuu wa Chuo Dkt. Prosper Mgaya (kushoto) akikabidhia vitabu na Meneja wa Kampuni ya Simba Supply Chain Solutions Ndg. Ajuaye Kheri Msese vinavyoelimisha umuhimu wa kubadili tabia kwa watumiaji wa Barabara "Mfumo Mahiri wa Msingi wa Kitabia" mara baada ya kuhuisha Mkataba wa Ushirikiano baina yaTaasisi hizo mbili, tarehe 4 Juni, 2024.
50 YEARS NIT ANNIVERSARY 1975-2025
Excellence in Transport for a Sustainable Economy.